UTAKATIFU

Image result for holinessNa Mwalimu Elishama Hubi
Utangulizi
Ndugu Mpendwa neno Mtakatifu ni pana sana kulifahamu, na kila MTU analijua kwa namna yake huyu hivi na huyu vile. Lakini kwa kadri ya ufunuo ulioko ndani yangu somo hili  hatuwezi kujifunza hata 1/8 ya somo kwa siku hata kwa wiki. Kwa Leo naomba tutafakari kwa pamoja sehemu ya utangulizi tu na ninaamini Mungu ataweka ari ndani yako ya kuendelea kujifunza zaidi juu ya somo muhimu sana la utakatifu.

UTAKATIFU ni tabia pekee ya Mungu inayoelezea jumla ya sifa, utendaji na uwepo wake. Hakuna tabia nyingine ambayo ni kuu kuliko UTAKATIFU kwa Mungu wetu.
Wanadamu tunampa Mungu sifa nyingi sana, ana upendo, ni mwema, ana huruma, ana Neema, ni mpole, ana nguvu, ni mkuu, na nyingine nyingi sana lakini UTAKATIFU ni Sifa pekee na Tabia kuu ya Mungu inayozaa sifa zote tumpazo Mungu.
Sifa zote tumpazo Mungu, ibada zote tumpazo Mungu, shukrani na heshima tumpazo Mungu, zote ni kwa sababu yeye ni Mungu Mtakatifu.
Ukisoma katika kitabu cha Isaya 6:3Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni BWANA wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake.
Zingatia "Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu........... Utukufu wako"
Biblia haijasema, mwema, mwema, mwema, au mwenye upendo, mwenye upendo, mwenye upendo, wala mpole, mpole, mpole,au mkuu, Mkuu, mkuu. Bali Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu.

Zingatia yafuatayo kabla hatujaendelea:
ü  Standard ya maisha katika ufalme wa Mungu ni UTAKATIFU.
ü  Wote watakaoingia katika ufalme wa Mungu lazima wawe watakatifu, yaani tiketi ya kuingia mbinguni ni utakatifu.
ü  Uhalali wa mwanadamu kutembea na Mungu ni UTAKATIFU.
ü  Kila kitu kitumikacho kwa ajili ya Mungu lazima kiwe kitakatifu, hata kikiwa kichafu kwa asili lazima kiwekwe wakfu kwa ajili ya Mungu.

Soma vifungu vifuatavyo;
 1 Petro 1:16kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
 Waebrania 12:14Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;
Zaburi 16:3Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.

Neno UTAKATIFU linaweza kutazamwa katika mitazamo mingi sana.
*     Utakatifu kama wito. (Calling)
*     Utakatifu kama Viwango(Quality)
*     Utakatifu kama Mchakato(Process)
*     UTAKATIFU kama Hali(Condition)
*     Utakatifu kama Tukio(Event)

UTAKATIFU KAMA WITO
Mungu anapokuita anakuwa na sababu mahususi juu yako binafsi. Na wito ni Mchakato. Wito wa Mungu mkuu kwa wanadamu ni kuwaita wote walioridhia kuwa RAIA wa ufalme wake na warithi wa ufalme kama wana wake wazaliwao si kwa mwili Bali kwa roho. Kwakuwa wote wanaoitwa na Mungu huzaliwa tena kwa roho na biblia inasema kilichozaliwa kwa mwili ni mwili na kilichozaliwa kwa roho ni roho.
Yohana 1:12-13Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.
Yohana 3:6Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
Mungu anapokuita anakusudia wewe kuwa RAIA wa ufalme wake. Mwana mteule.
Lakini kuna ‘process’ unapitia kufikia kiwango cha kuwa mtimilifu kwakuwa UTAKATIFU ni ‘process’ .
 Efeso 4:11-13Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;

Wengi wanajua kabisa kwamba Mungu anapokuita anahitaji ufanye kazi yake kama uchungaji, ualimu, uimbaji n.k lakini ukweli ni kuwa hizo huduma ni Mchakato wa kulikamilisha kusudi .
Kusudi la wito  ni :
ü  kuwakamilisha watakatifu
ü  kazi ya huduma itendeke
ü  mwili wa Kristo ujengwe.

Hivyo ili kufikia kiwango hicho UTAKATIFU kama WITO unapitia hatua  hizi;
Ø  WITO
Ø  Kufanywa mwana
Ø  Kupokea tabia ya baba
Ø  Kuishi kwa ‘Standard’ ya ufalme
Ø  Kulitumikia kusudi

Rum 8:14Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu.
 Ili kulikamilisha kusudi LA Mungu, Utakatifu unatakiwa uwe sehemu ya maisha yako.

Living Holy is achieved through kingdom standard States which involves the Listening, Accepting and Practicing the Word of God you hear during God's calling.
It involves your personality ie Spirit, Soul (mind, will, emotions), Body.
  • Mindsets
  • Attitude
  • Habits
  • Character
  • Living
Mindsets are maps for our living. They shape our attitude which influences habits and behaviours that in turns describes our character.
Unapolisikia Neno la wito wa Mungu lazima uwe na ‘right mindsets’ ili kukujengea ‘attitude’ itakayokupa ‘the best habits.’
Tabia hizo ndizo zile zinazompa Mtakatifu utukufu wake.  Kanuni ya maisha matakatifu ni kuongozwa na roho Mtakatifu. Kwakuwa hakuna maisha bila roho hivyo maisha matakatifu bila roho Mtakatifu hayawezekani.
Kwakuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu hao ni wana wa Mungu.
Ndugu Mpendwa katika utangulizi huu naomba kuhitimisha kwa kusema yafuatayo:
ü  Kabla ya kitu chochote unatangulia Utakatifu.
ü  Mungu anatuita tukiwa waovu ili tuwe watakatifu.
ü  Kabla ya huduma yako Mungu anataka UTAKATIFU kwanza.
ü  Kabla ya maisha yako Mungu anataka UTAKATIFU kwanza
ü  Kabla ya mafanikio yako Mungu anataka UTAKATIFU

Kwanini?
Kwa sababu kwa UTAKATIFU wake dunia yote inajaa utukufu wake na aliahidi utukufu wake hatampa mtu mwingine Isaya 42:8 Mimi ni BWANA; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.

Katika ufalme wa Mungu ulio katika asili ya UTAKATIFU tunatafuta usahihi wa vitu kabla ya kuvifanya kwa usahihi. ‘Doing right things before doing things right.’ Mungu hataki  umtumikie Bali anataka utumikie kusudi lake sahihi Kumbuka ‘Abuse is inevitable if the Right purpose is unknown.’

Utakatifu sio ule  tu unaoonekana kwa nje  Bali hata ule  wa ndani usioonekana. Mambo Yale unayoyafanya ukiwa mwenyewe, chumbani kwako au popote pa siri, Mungu anayachunguza Sana. Na anayemheshimu Mungu Toka sirini Mungu anamheshimu sana.

 UTAKATIFU sio cheo, wala kitu cha kusomea, wapo wanaoamini kuwa kusoma bible school, kuwa Mchungaji, askofu, padre sister kwamba ndo UTAKATIFU sio kweli . UTAKATIFU ni wito wa Mungu.

 UTAKATIFU sio wa rika Fulani. Wapo wasemao Vijana hawawezi kuwa watakatifu, kwani vishawishi ni vingi, wengine wanasema mimi nitakuwa Mtakatifu nikioa au kuolewa, au nikizeeka.  Huko ni kujidanganya mwenyewe.
Utakatifu ni wa kila mtu na ni hapa duniani. Wapo wasemao hakuna watakatifu duniani hayo ni mawazo ya kibinadamu kwani Mungu mwenyewe kasema anapendezwa na watakatifu walioko duniani.

Tabia hizi ni lazima  kwa kila Mtakatifu:
*     Kusoma neno na kuliishi.
*     Kuomba kila siku
*     Kuongozwa na Roho Mtakatifu,
*     Kulitumikia kusudi sahihi na
*     Kujitoa kwa Mungu kwa hali na mali

Hata wewe una haki ya kuwa mtakatifu, kama tu utakubali wito na kukubali kuishi katika kusudi la Mungu.”

‘To experience holy life is hard But Not Living holy is harder.
In order to live a life you never lived before you need to pay a cost you never paid before and acquire knowledge you never acquired before.’


Previous
Next Post »