Tatizo sio kwamba hatuwezi kufanya ila tatizo ni kwamba hatutaki kukubali udhaifu wetu nรฃ kuwaruhusu tu wale wanaoonekana kuwa hodari katika hilo wakalifanya hilo, tatizo ni kwamba tunajiamini kuwa tuko perfect katika kila jambo tunasahahu ya kuwa sisi ni mwili wa kristo .. Kila mmoja anaweka jitihada ya kufanya vema sio kama wajibu ila ni ili aonekane kuwa bora kuliko fulani, tunasahau kuwa biblia inasema tuwahesabu wengine kuwa ni borรก kuliko sisi. siรด kwamba tunashindwa kujenga Gorofa uwezo tunao ila tatizo ni Kwamba kila mtu anataka ajenge msingi.. Siรด kila kiungo Katika mwili chaweza kuonekana viungo vinginรฉ katika mwili havionekani na kutokuonekana kwake hakumaanishi kuwa viungo hivyo havina umuhimu, wakati mwingine vyaweza kuwa nรฃ umuhimu kuliko hata vinavyoonekana ...
Yamkini wewe ni moyo, au ni kwapa ๐๐๐ . Hapo ndipo umeitiwa sasa usijilazimishe kuwa jicho uonekane maana yeye aliyekuweka hapo kakuweka kwa kusudi..
Kila mtu kuna huduma Mungu kamuitia kwayo,
Inaweza kuwa inafahamika kwa watu wengi au haifahamiki, lakini kufahamika au kutokufahamika hakudetermine ukubwa wa huduma..
Yamkini watu hawakujui lakini kuna kazi kubwa sana unaifanya katika kuujenga ufalme wa Mungu. Nรฃ kupitia hiyo Mungu anajivunia..
Lengo langu katika ujumbe huu ni hili..
Kila mtu amuhesabu mwenzake kuwa ni borรก kuliko yeye.. Nรฃ tusifanye huduma kwa mashindano kwa nia ya kuonekana kuwa borรก kuliko fulani.. Ila tufanye kama viungo katika mwili wa kristo.. Mwingine anapoinuliwa basi kusiwe nรฃ wivu ila furaha nรฃ shukrani kwasababu aliyeinuliwa ni kiungo ndani ya mwili wa kristo.. Mwingine anapoanguka isiwe chanzo cha kuthibitika kwa unabii ila kila mmoja asikie kuugua juu ya anguko la kiungo ndani ya kristo.. Kama vile ilivyo katika mwili kidole kikiumia mwili wote huuma .
Tusipopendana sisi kwa sisi hatuwezi kumpenda Mungu.. Sababu Mungu ni Pendo..
Tupendane tuchukuliane, tusameheane.. Hakika tutafika..
Kila mtu amkubali tu mwenzake katika eneo au karama Mungu aliyompa.. Kama wewe ni muhubiri basi fanya iliyo nafasi yako.. Kama wewe ni pianist vivyo hivyo.. Sasa sio unakuta pastor ndo muimba kwaya.. Ndo muhazini wa kanisa, ndo pianist wa kanisa, ndo mshauri, mwalimu.. Muinjilisti etc nooo.. Hatuwezi kuwa perfect katika kila eneo.. Maeneo Mengine tuwaachie wale wenye wito huo wakafanya๐๐
Ubarikiwe
Waweza like page yangu Judith Mbilinyi kwa kujifunza zaidi au
0762372408
judithmbilinyi@gmail.com
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon