Namna tunaishi na jamii ya kanisani ingefanana na namna tunaishi na jamii inayotuzunguka nje ya kanisa tusingehitaji kushuhudia, kwa matendo yetu wangevutwa. Tusipowapenda majirani, tukasema tunampenda Mungu tunajidanganya wenyewe. Kipimo cha kumpenda Mungu kimefungwa kwenye kumpenda jirani. Hatuwezi kuwa watoaji kanisani tusiwe watoaji kwa jamii inayotuzunguka. Hatuwezi kuwa na heshima kwa walezi wetu kanisani tukashindwa kuheshimu wazazi wetu nyumbani, hatuwezi kuwa na kauli nzuri kanisani tukashindwa kuwa na kauli nzuri nje ya kanisa. Ibada sio kanisani pekee, namna tunaishi Leo ni ibada kwa Mungu. Amua kuwa halisi.
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon